Staa wa Muziki wa Kizazi Kipya Bongo,Rehema Chalamilla 'Ray C', akiingiza sauti ndani ya Studio za THT,
chini ya maproducer Emma The Boy na Tudy Thomas,ambao wamepania
kumrejesha katika game kwa kishindo msanii huyo, ambaye alipotea kwenye
ulimwengu wa Burudani baada ya kutopea katika utumiaji wa madawa ya
kurevya ambayo kwa sasa ameachana nayo na kumrudia mwenyezi Mungu
sambamba na kuendelea kutumia dozi ya kuondoa sumu ya madawa hayo.
Ray C akiingiza sauti tayari kwa maandalizi ya ujio mpya kwenye game la Bongo Fleva.
Producer Tudy
Thomas (kulia), akicheka jambo lililotokana na majadiliano ya kuboresha
ngoma mpya ya Rey C, wa kwanza kushoto na katikati ni Emma The Boy
akipiga mzigo tayari kwa kumkamilishia Ray C ngoma yake mpya ambayo
anatarajia kuiachia hivi karibuni baada mara tu itakapo toka mikononi
mwa Maproducer hao.
Ray C, akijalibu kutoa akapela kwa Maproducer hao, wakati wakiendelea kuiboresha ngoma yake mpya.
No comments: