Friday, September 27, 2013

RAY C AAMUA KUTOKA SASA CHEKI PICHA HAPA

Staa wa Muziki wa Kizazi Kipya Bongo,Rehema Chalamilla 'Ray C', akiingiza sauti ndani ya Studio za THT, chini ya maproducer Emma The Boy na Tudy Thomas,ambao wamepania kumrejesha katika game kwa kishindo msanii huyo, ambaye alipotea kwenye ulimwengu wa Burudani baada ya kutopea katika utumiaji wa madawa ya kurevya ambayo kwa sasa ameachana nayo na kumrudia mwenyezi Mungu sambamba na kuendelea kutumia dozi ya kuondoa sumu ya madawa hayo.
Ray C akiingiza sauti tayari kwa maandalizi ya ujio mpya kwenye game la Bongo Fleva.

Producer Tudy Thomas (kulia), akicheka jambo lililotokana na majadiliano ya kuboresha ngoma mpya ya Rey C, wa kwanza kushoto na katikati ni Emma The Boy akipiga mzigo tayari kwa kumkamilishia Ray C ngoma yake mpya ambayo anatarajia kuiachia hivi karibuni baada mara tu itakapo toka mikononi mwa Maproducer hao.
Ray C, akijalibu kutoa akapela kwa Maproducer hao, wakati wakiendelea kuiboresha ngoma yake mpya.

No comments:

Speak Your Mind

Powered By Blogger · Designed By Seo Blogger Templates